KAULI YA ZIIKI MEDIA KUHUSU KERO ZINAZOIBULIWA NA WASANII

Hivi majuzi, wasanii wetu wamelalamika kwenye mitandao kuhusu mabadiliko kwenye kanuni ya kutoa muziki yao. 
Ingawa Ziiki ina wajibu kimkataba kutofichua maelezo ya Mikataba yetu na wasanii, ni muhimu kufafanua msimamo wetu kwenye suala hii. Ziiki Media inajitofautisha kama kampuni inayoongoza kwenye usambazaji wa muziki wa kidijitali. 

 Ziiki inashirikiana na kampuni zaidi ya 200 za kidijitali, na kampuni za mawasiliano ya simu ili kusambaza na kuchuma mapato ya maudhui ya wasanii katika umbo la sauti na video.


 Ziiki pia ina ushirikiano na kampuni inayoongoza muziki ulimwenguni, Warner Music Group (WMG) kutekeleza majukumu haya. Lengo letu siku zote limekuwa kuinua na kuwezesha mafanikio ya wasanii wetu humu Africa na kote ulimwenguni. 
Ili kufanikisha lengo hili, tumeandaa miongozo mbalimbali na kuwasilisha miongozo haya kwa wasanii na wadau wetu. 

 Pamoja na upanuzi wa fursa zinazoongezeka katika soko la kidijitali na kimataifa, fursa na matarajio ya sasa yaliyowekwa kwa tasnia ya muziki ya Afrika Mashariki hayawezi kuwekewa mipaka katika eneo pekee. Kama kampuni tunafanya kazi bila kuchoka kufungua soko la kimataifa la wasanii wetu, na kwa hivyo lazima tusisitize mbinu bora zinazopaswa kupitishwa na wasanii wote ulimwenguni, pamoja na wale kutoka Afrika Mashariki.
Makamu wa Rais wa Operesheni wa Ziiki Media, Abhinandan Bhardwaj ameeleza kuwa 

Mikataba ya wasanii wetu yanashugulikia wasilishaji na utoaji wa nyimbo.Kwa kutia sahihi katika hiyo mikataba, wasanii wetu wamethibitisha kuwa wanakubaliana na masharti yake. Mojawapo ya maswala ambayo Ziiki Media inakabiliana nayo ni wasanii wakati mwingine kuwa na uelewa mdogo wa jukumu muhimu la wakati katika usambazaji wa muziki.

 

” Katika enzi ambapo upesi hutawala, umuhimu wa kuruhusu muda wa kutosha kwa mchakato wa usambazaji unaweza kupuuzwa. Bwana Bhardwaj anasisitiza, "Kama vile utunzi unavyofunua juu ya mienendo tofauti, mchakato wa usambazaji unahitaji mwendo wa uangalifu. Kukimbia kunaweza kunyamazisha bila kukusudia athari tunayokusudia kuunda." Kama msambazaji aliyeidhinishwa, maudhui yote lazima yawasilishwe kwa timu ya Ziiki na baadaye yatayarishwe kupakiwa kwenye zaidi ya majukwaa 200 duniani kote. Timu katika Ziiki Media hufanya kazi kwa karibu sana na wasanii na timu zao ili kuhakikisha kuwa maonyesho yao ya juu zaidi yanapatikana kwa matoleo yao. Taratibu hizi zinatumia muda, na hivyo kulazimisha kipindi cha notisi kilichobainishwa katika makubaliano ya wasanii. Toleo lolote la muziki lisilopangwa huingilia muda uliokubaliwa na kuathiri biashara vibaya.

 

Ziiki Media inasimamia kujitolea kwake kukuza vipaji vya kisanii, kukuza uvumbuzi, na kuwawezesha wasanii kufikia uwezo wao kamili. Tumejitolea kufanya kazi kwa karibu na wasanii wetu wote na timu zao ili kuunda mazingira ambayo yanahimiza ubora wa ubunifu huku tukihakikisha mbinu ya kimkakati ya matoleo ya muziki.

 

Tunachukua fursa hii kuwashukuru wasanii wetu wote, washirika, serikali, mashirika ya udhibiti ambao wametuunga mkono kwa miaka mingi. Kwa niaba ya wadau wetu, tunathibitisha dhamira yetu ya kuboresha mfumo wa muziki katika Afrika Mashariki na kwingineko.

No comments

anonymous