SIKU 100 ZA RAIS SAMIA, MRADI CHALINZE WAKAMILIKA
Katika siku 100 za Mh Rasi Samia Suluhu Hassan, Wanachalize wafurahia juhudi za Mbunge wao Ridhiwani Kikwete kwa kukamilisha ujenzi wa soko lilogharimu Fedha za kitanzania milioni 400.
Soko hilo ni sehemu ya Mradi uliokusudiwa na Mh. Rais Samia, ili kuwafikia wananchi wa hali ya chini na kujipatia kipato.
Soko litakapo kamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua wafanya biashara zaidi ya 120, na lipo Chalinze Mjini njia ya kuelekea Magidu.
Mbunge Ridhiwani Kikwete anawakaribisha watanzania Jimboni kwake ili kuona miradi mbalimbali aliyoweza kukamilisha kwa kipindi chote alichopewa ridhaa na wanachalinze.
Post a Comment